Timu ya Yanga ndiyo inaongoza kwenye msimamo Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2022/23 ikiwa na jumla ya pointi 56 wakiwa wamecheza mechi 21, bado mechi 9 wakati watani zao Simba wakiwa nafasi ya pili na pointi zao 50.
Kimahesabu kama Yanga wakishinda katika mechi zao (7) zijazo na kupata sare (01) au ashinde mechi 8 na kupoteza moja, watatwaa Ubingwa wa (29) wa Ligi Kuu Tanzania Bara hata kama Simba atashinda mechi zake zote.
1▪️Namungo - Mkapa!
2▪️KMC - Mkapa
3▪️Geita Gold - Mkapa
4▪️Kagera Sugar - Mkapa
5▪️Singida Big Stars - Liti
6▪️Dodoma jiji - Mkapa
7▪️Simba - Mkapa
8▪️Mbeya City - Sokoine
Ikitokea wapinzani wao wakuu 'Simba' wakatoa sare au kupoteza mchezo, michezo wanayohitaji Yanga kushinda ili wawe mabingwa itapungua zaidi. Zimesalia mechi tisa kumalizika.
Nani unampa nafasi ya kutwaa Ubingwa huo.