Mon, 15 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa wa Kombe la Dunia mwaka 2010, Timu ya Hispania iliwapasa mpaka wasubiri dakika za jioni kujihakikishia tiketi ya kwenda kushiriki kwa Fainali za Kombe la Dunia nchi Qatar 2022.
Bao pekee la Alvaro Morata zikiwa zimesalia dakika nne limeipa Hispania tiketi ya Kombe la Dunia mwakani Qatar baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Sweden usiku wa kuamkia leo katika mchezo wa Kundi B Uwanja wa OlĂmpico de Jijini Sevilla.
Hispania inamaliza na pointi 20, tatu zaidi ya Sweden inayokwenda kucheza Play-Off kujaribu tena kukata tiketi ya Qatar.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live