Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hiki kingewapata Namungo FC

Namungo Pic 2 Data Hiki kingewapata Namungo FC

Fri, 19 Feb 2021 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Gumzo kubwa wiki hii lilikuwa likihusu timu ya Namungo FC ambayo ilitua wiki iliyopita nchini Angola kwa ajili ya pambano la Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya CD de Agosto ya huko. Mara baada ya kutua nchini humo wachezaji wote walitakiwa kuwekwa karantini katika hoteli waliyofikia wakielezwa kuwa vipimo vinaonyesha kuwa watatu kati yao wana maambukizi ya Covid-19.

Hata hivyo, Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limeifuta mechi iliyokuwa ichezwe Jumapili kutokana na tukio hilo ambalo lilileta taharuki kwa pande zote mbili.

Kwa upande wa uamuzi wa kuifuta mechi hiyo inaweza kuwa ni faida kwa Namungo FC - hii ni kutokana na namna walivyofanyiwa mara baada ya kuambiwa wabaki tu hotelini.

Tukio kama lile la kuwekwa wote karantini kwa ghafla lingeweza kuwaathiri kisaikolojia na hata ingetokea wakacheza mechi na timu hiyo, ingeathiri kiwango chao cha uchezaji.

Kuhudumiwa kwa namna ile kama vile sio binadamu kunaweza kuwapa wachezaji mpasuko wa hisia na hatimaye wakakosa furaha na kuwa wanyonge, hivyo ingekuwa vigumu kucheza kwa kujiamini.

Hali kama ile ni kawaida pia kuwakuta wachezaji wakiwa katika hali ya hofu au woga na kupata msongo wa mawazo vingeweza kuwapata wachezaji hao pamoja na viongozi walioambatana nao.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz