Fri, 10 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa masuala ya soka nchini George Job, ametaja kiini cha sintofahamu inayoendelea katika Klabu ya Simba SC kuwa ni uchaguzi.
Amesema timu hiyo ni kama haikumaliza makundi mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa viongozi wa klabu hiyo.
“Kiini cha haya yanayoendelea sasa Simba ni Uchaguzi Mkuu uliopita, watu walikuwa wanatafuta sababu ya kutoa nyongo zao lakini waliikosa sababu na muda wakufanya hivyo.
“Haya malalamiko ya sijui hawamtaki Mangungu na viongozi wengine kiini chake ni uchaguzi Mkuu kwa sasa ni muendelezo tu.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live