Wed, 3 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa mchambuzi wa masuala ya soka kupitia Efm na TVE, Geof Lea amejiunga na kituo cha Crown FM inayomilikiwa na msanii Alikiba.
Crown FM Radio imeanzisha kipindi cha michezo ambacho kinaitwa Crown Sports na kitakuwa kinaruka hewani kuanzia saa (3) asubuhi mpaka saa (6) mchana.
Watangazaji na wachambuzi ni:
◉ Geof Lea
◉ Hans Raphael
◉ Naseeb Mkomwa
◉ Pablo Almas
◉ Juma Ayo
Inaelezwa kuwa, Jemedari Said pia yuko kwenye mazungumzo ya kujiunga na kituo hicho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live