Je, unajua kuwa Klabu ya Petro de Luandaya Angola, msimu huu wachezaji wao wa kigeni hawatoki Katika Bara la Afrika?
Kwenye Kikosi chao Wana Wareno watatu, Wabrazil wawili, na kutoka Honduras mmoja na wachezaji wengine waliobaki wanao unda Kikosi Cha Mreno Alexander Santos wote ni raia wa Angola.
Msimu Huu kwenye #CAFCL Wapo Kundi 'C' Pamoja na timu za Al Hilal, Etoile Sahel na Esperance Tunis.
Wamempiga Al Hilal (1-0) na wameenda Tunisia na kuifunga Etoile Sahel (2-0) na kutoka sare (0-0) na Espérance Tunis, wanongoza Kundi wakiwa na alama 7, Kumbuka Hawajaruhusu Goli Hadi sasa.
Wamewekeza sana ndani ya Uwanja na kuunda Kikosi kinacho endelea kuhimalika siku Hadi siku, Petro de Luanda ni tatizo kwenye #TotalEnergiesCAFCL msimu Huu.