Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hii ndiyo jezi atakayovaa Mbappe Madrid

Mbappe 660x330 1 Hii ndiyo jezi atakayovaa Mbappe Madrid

Wed, 21 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Real Madrid imeripotiwa kumwaandalia supastaa Kylian Mbappe jezi yenye Namba 10 mgongoni wakati atakapojiunga nao kwenye majira yajayo ya kiangazi akitokea Paris Saint-Germain.

Mbappe amekuwa akihusishwa na mpango wa kwenda kujiunga na miamba ya Santiago Bernabeu kwa miaka michache ya karibuni, ikiwamo kwenye dirisha lililopita la majira ya kiangazi.

Mshambuliaji huyo Mfaransa aliwekwa nje ya kikosi cha Paris Saint-Germain kwa muda baada ya kuiambia klabu hiyo kwamba hana mpango wa kuongeza mwaka zaidi wa kuendelea kubaki kwenye kikosi hicho.

PSG ilifanya jaribio la kumuuza mshambuliaji huyo mwaka jana, lakini ilishindwa kufanya hivyo kabla ya kumruhusu kuitumikia tena timu hiyo ya kocha Luis Enrique na kiwango chake cha sasa ni moto balaa.

Wakati dili lake la sasa likitarajiwa kufika ukingoni Juni, Mbappe alimwambia Rais wa PSG, Nasser Al-Khelaifi kwamba ataachana na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Ripoti zaidi zinadai kwamba Rais wa Real Madrid, Florentino Perez aliwaambia mastaa wa kikosi cha kwanza cha Los Blancos kwamba Mbappe atajiunga nao bure kwenye dirisha lijalo la usajili.

Wakati huo, Mbappe amekuwa ahihusishwa pia na klabu za Ligi Kuu England, lakini kinachoonekana mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 22, ataondoka Paris kwenda Madrid kwa ajili ya msimu ujao.

Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, Real Madrid imejiandaa kumpa Mbappe jezi Namba 10 atakapokamilisha uhamisho wake wa kutua Santiago Bernabeu.

Kwa sasa staa huyo huko PSG anavaa jezi Namba 7 ambayo kwenye kikosi cha Los Blancos inavaliwa na Vinicius Junior, na Mbrazili huyo hana mpango wa kuiachia.

Na sasa Mbappe atakwenda kurithi Namba 10 kutoka kwa kiungo Luka Modric, ambaye mkataba wake huko Real Madrid utafika ukomo mwishoni mwa msimu huu.

Modric amekuwa na wakati mgumu katika kupata namba msimu huu na kutokana na hilo bila ya shaka itakapafika mwisho wa msimu huu itakuwa mwisho kwake. Kwa msimu huu, Mbappe amefunga mabao 32 mechi 31 za kimashindano.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live