Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Soka Tanzania TFF, imethibitisha kuwa haikuihusisha klabu ya Azam katika mchakato wa Kocha Bora wa mwezi Novemba, kutokana na kutokuwa na Kocha Mkuu katika mwezi huo.
Ufafanuzi huo unakuja baada ya Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Soka Tanzania TFF kutangaza majina ya mchezaji bora wa mwezi Novemba ambayo imekwenda kwa Mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele na Kocha Bora akiwa ni Juma Mgunda kutoka Simba SC.
Kuna waliiona kuwa tuzo hiyo haikustahili kwenda kwa Mgunda kwa sababu Kally Ongala amefanya vizuri mwezi Novemba akiwa na Azam FC akicheza michezo mitano na kushinda michezo yote.