Mchambuzi wa soka, Hans Raphael amesema, Gamond alitambua uwezo mkubwa wa Aziz Ki lakini alimuacha hadi alipokuja kuiamua mechi.
"Siku zote makocha wakubwa duniani huweka Imani kwa wachezaji wao wakubwa,Inawezekana siku husika mchezaji akawa na siku mbaya kazini,au kiwango chake kikashuka ghafla lakini kwa namna yeyote kocha atambakisha uwanjani huku akiamini mchezaji mkubwa anahitaji moment moja kuamuwa mechi.
Aziz Leo hakuwa na mchezo mzuri,amepoteza baadhi ya nafasi Ila Gamond,alijua kuna moment itafika Aziz atafunga…..Mwisho wa siku ndicho kilichotokea.
Cut back nzuri ya Pacome,Finishing bora ya Aziz…Tayari Yanga wako fainali na Azam Fc."