Droo ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika imetoka ambapo vigogo 16 waliofuzu hatua hiyo wakibaini wapinzani wao.
Vigogo wa London, Arsenal wamepangwa dhidi ya miamba ya Ureno FC Porto huku Mabingwa watetezi, Manchester City wakipangwa dhidi ya wababe wa Manchester United, FC Copenhagen.
Mabingwa wa kihistoria wa ligi hiyo, Real Madrid wamepangwa dhidi ya vigogo wa Ujerumani, RB Leipzig huku FC Barcelona ikikutanishwa na Mabingwa wa Italia, Napoli.
Inter Milan ya Italia imepewa mfupa mgumu baada ya kupangwa dhidi ya vigogo wa Uhispania, Atletico Madrid huku PSG ya Ufaransa ikipewa Real Sociedad ya Uhispania.
DROO KAMILI
Copenhagen vs Man City
RB Leipzig vs Real Madrid
Porto vs Arsenal
Napoli vs Barcelona
PSG vs Real Sociedad
Inter vs Atletico Madrid
PSV vs Dortmund
Lazio vs Bayern Munich
Chama lako limepangwa na nani?