Mon, 12 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imepangwa kundi C katika droo ya Ligi ya Mabingwa Afrika iliyofanyika leo nchini Misri.
Katika kundi hilo C, Simba imepangwa na timu za Raja Casablanca (Morocco), Horoya (Guinea) na Vipers (Uganda).
Mechi za mzunguko wa kwanza hatua ya makundi zitaanza kupigwa Februari 10 na Februari 11, 2023.
Mtiririko mzima wa makundi upo kama unavyoonekana hapa chini;
KUNDI A: Wydad AC Petro Atletico JS Kabylie AS Vita
KUNDI B: Al Ahly Mamelodi Sundowns Al Hilal Coton Sport
KUNDI C: Raja CA Horoya AC Simba Vipers
KUNDI D; Esperance Zamalek CR Belouizdad Al Merrikh
Chanzo: www.tanzaniaweb.live