Wed, 10 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa Arsenal, William Saliba na Bukayo Saka wameteuliwa kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashindano ya Euro 2024, pamoja na orodha ya wachezaji wengine.
Waliojiunga nao ni Rodri, Cody Gakpo, Jude Bellingham, Lamine Yamal, Fabián Ruiz, Kylian Mbappé, N'Golo Kanté, Nico Williams na Dani Olmo.
Cha kufurahisha, Antoine Griezmann (EURO 2016) ndiye mchezaji pekee aliyeshinda tuzo hii bila kunyanyua kombe la mashindano.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live