Sun, 5 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa wa Tanzania, Simba SC wamefanikiwa kufuzu Hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya kuchapwa mabao 2-1 na wenyeji, Red Arrows jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Mashujaa Jijini Lusaka, Zambia.
Mabao ya Red Arrows yamefungwa na Ricky Banda dakika ya 45 na Sadam Phiri dakika ya 48, wakati bao pekee la Simba SC limefungwa na Kiungo Hassan Dilunga dakika ya 67.
Simba SC inaingia hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa 4-2 kufuatia kushinda 3-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Dar es Salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live