Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wamemtambulisha kocha mpya wa Makipa Chlouha Zakaria ambaye atakuwa na kazi ya kuwanoa makipa wa klabu hiyo.
Kabla ya kumtambulisha, jana Jumatatu, Meneja wa Habari wa klabu hiyo, Ahmed Ally aliweka bayana kuwa, kabla wiki hii haijaisha, watambulisha kocha huyo wa makipa.
Kabla ya kumtambulisha kocha huyo, Simba walikuwa wakimtumia Muharami Said Mohammed kama kocha wa muda wa makipa na leo hii, amekumbwa na kashfa ya kudaiwa kukutwa na madawa ya kulevya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live