Wed, 29 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa Kimataifa wa Taifa Stars na klabu ya Simba SC, John Bocco ametangaza kustaafu soka baada ya kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara kwa zaidi ya Misimu 16.
Bocco ndiye mchezaji mwenye magoli mengi katika Historia ya mpira wa miguu Tanzania. Kwani amefanikiwa kufikisha Mabao 154. mbele ya mwamba Mohammed Mmachinga mwenye Magoli 152.
Yote kwa yote huyu Mwamba hapaswa kuagwa kizembe kwani ni miongoni mwa Watu walioweka rekodi ndani ya Ligi kuu hapa Tanzania Bara.
Kila la kheri Legend kwenye Majukumu yako mapya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live