Tue, 26 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji Dani Alves ameachiliwa kutoka Gerezani baada ya kulipa dhamana ya Euro Milioni Moja akisubiri baada ya kukata rufaa kuhusu kesi ya ubakaji.
Dani Alves anashutuhumiwa kwa ubakaji na ambapo alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka minne na nusu Gerezani kabla ya kuomba kutoka kwa dhamana.
Baada ya nyota huyo wa zamani wa kandanda ambaye amewahi kukipiga katika timu za Barcelona na Paris Saint-Germain, kuachiliwa kwa dhamani kutoka gerezani, atakuwa anaripoti Mahakamani akiwa anatoka katika nyumba yake ya kifahari iliyopo Esplugues karibu na mji wa Barcelona.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live