Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hat Trick ya Mayele yairudisha Yanga kileleni Ligi Kuu NBC

Mayele 3.jpeg Fiston Mayele aliweka wavuni mabao matatu

Fri, 18 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mabingwa watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Singida Big Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mchezo uliopigwa Uwanja wa Benjamin Jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga SC yamefungwa na mshambuliaji wake kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Fiston Kalala Mayele matatu, dakika za 16, 27 na 56 na beki wa pembeni, Kibwana Shomari dakika ya 48, wakati la SBS limefungwa na mkongwe, Meddie Kagere dakika ya 66.

Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 26 katika mchezo wa 10 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi tu wastani wa mabao Azam FC ambayo pia imecheza mechi mbili zaidi, wakati Simba SC yenye pointi 24 za mechi 11 inashukia nafasi ya tatu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live