Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hat-Trick ya Man United yampa mkataba Foden

Phil Foden Contract Phil Foden

Tue, 4 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Phil Foden anaripotiwa kusaini mkataba mpya na Man City mapema wiki hii, baada ya kuonesha mchezo mzuri kwenye mechi yao ya dabi kwa kufunga hat-trick yake nzuri na ya kwanza dhidi ya Manchester United.

Foden alizidi kuwa shujaa akiwa City baada ya kufunga hat-trick yake ya kwanza katika maisha yake ya soka dhidi ya wapinzani wake katika ushindi wa 6-3 dhidi ya Manchester United siku ya Jumapili.

Kwa kufanya hivyo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 alifikisha mabao 50 chini ya Pep Guardiola, akiwa na umri mdogo hata kuliko Lionel Messi.

Na habari njema inatazamiwa kuendelea, huku City wakitumai kuwa Foden ataweka bayana kwenye mkataba wake mpya mapema wiki hii kufuatia mazungumzo marefu na klabu hiyo, kwa mujibu wa The Athletic.

Mshambuliaji huyo ambaye ni kijana wa ndani na shabiki wa City, hajawahi kufikiria kuondoka Etihad lakini mazungumzo ya kusaini mkataba mpya yalicheleweshwa kutokana na mabadiliko katika usimamizi wake.

Hata hivyo, mkataba sasa unakaribia kuthibitishwa, The Athletic iliripoti, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 akitarajiwa kusaini kwa miaka sita zaidi mara tu maelezo ya mwisho yatakapokamilika.

Mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika 2024 na Sportsmail iliripoti mnamo Agosti kwamba City walikuwa wamewasilisha ofa ya kuongeza mkataba wa miaka sita, wenye thamani ya paundi 225,000 kwa wiki.

Foden, ambaye alijiunga na klabu hiyo akiwa na umri wa miaka minne, alisaini udhamini wake wa kwanza wa akademi na klabu hiyo mwaka wa 2016 na kwa sasa thamani yake ni paundi milioni 132 hii ni kwa mujibu wa CIES Football Observatory.

Fowadi huyo wa Uingereza amepanda daraja Etihad, akicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Tottenham Hotspur akiwa na umri wa miaka 17 tu, huku pia akiwa mfungaji bora zaidi kuwahi kufunga katika klabu hiyo kwenye Ligi ya Mabingwa mwaka 2019.

Tangu wakati huo Foden, ambaye alishinda Tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa 2021 wa PFA, amekuwa mmoja wa wachezaji wadogo wanaotarajiwa katika soka la Ulaya, akiwa ameichezea City zaidi ya michezo 180, akifunga mabao 51 na kutoa pasi za mabao 35 katika mashindano yote.

Fowadi huyo ameshinda mataji manne ya Ligi Kuu akiwa na klabu hiyo katika maisha yake mafupi hadi sasa, ambayo tayari ni zaidi ya baadhi ya wachezaji wakubwa wamepata katika maisha yao ya soka.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live