Thu, 30 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa timu ya taifa ya England Harry Kane na mkewe Kate wanatarajia kupata mtoto wa nne.
Kupitia mtandao wa Instagram, Kane (29) ameposti picha akiwa na mkewe huku wakiwa wameshikilia kipimo cha ujauzito kinachoonyesha majibu chanya.
Posti hiyo iliambatana na ujumbe mfupi uliosema ”Tuna furaha kubwa kutarajia mtoto namba 4!”
Katika posti hiyo pia kuna video fupi inayoonyesha kiumbe hiko kikiwa tumboni. Video hiyo ina swali fupi lililouliza ” Ni jinsia gani?".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live