Fri, 8 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Manchester United, Rasmus Winther Højlund amechaguliwa kuwa Mchezaji bora wa mwezi Februari 2024 wa Ligi Kuu England.
Højlund ameshinda tuzo hiyo ya kufunga magoli manne na kusaidia (assist) goli moja kwenye mechi nne za Man United kwa mwezi Februari.
Højlund (21) raia wa Denmark alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kufunga katika mechi sita mfululizo za Ligi Kuu England mapema mwezi Februari.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live