Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gwiji wa zamani Liverpool, afariki akiwa na miaka 83

Roger Hunt Gwiji wa zamani wa Liverpool, Sir. Roger Hunt

Tue, 28 Sep 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Liverpool inaomboleza msiba wa Gwiji wake wa zamani Roger Hunt. Hunt alichezea Liverpool miaka takribani 50 iliyopita, lakini rekodi yake ya kupachika mabao kwenye Ligi Kuu ya England kwa mchezaji wa Liverpool bado haijavunjwa.

Mwaka 1966 alikuwa sehemu ya kikosi cha England kilichotwaa ubingwa wa Kombe la Dunia. Wiki mbili baadaye akajiunga na kikosi cha Liverpool kujiandaa na msimu mpya.

Roger Hunt anashika nafasi ya pili kwa wafungaji bora wa muda wote wa Liverpool akiwa amefunga magoli 285 akicheza michezo 492.

Roger Hunt aliezaliwa mwaka 1938 amefariki akiwa na umri wa miaka 83. Amewahi kufundishwa pia na Kocha Bill Shankly.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live