Tue, 21 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amewadokeza Waandishi wa Habari wakati wa mahojiano hapo jana baada ya Kutwaa taji la EPL kwa mara ya 4 mfululizo kuwa anampango wa kuondoka Klabuni hapo baada ya Msimu ujao wa 2024-25 kutamatika.
“Ukweli ni kuwa nipo karibuni kuondoka ndani ya Manchester City. Tayari nimezungumza na Viongozi na kuwaweka bayana kuwa bado nitaendelea kwa Msimu ujao ila tutafanya mazungumzo tena katikati ya Msimu huo.
"Nina mkataba na ninafuraha kuwa hapa Man City msimu ujao, kabisa! Nabaki hapa City,” alisema Guardiola.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live