Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Granit Xhaka: Mikel Arteta anatosha Arsenal

Image 715.png Granit Xhaka: Mikel Arteta anatosha Arsenal

Wed, 24 May 2023 Chanzo: Dar24

Kiungo wa kati wa Arsenal, Granit Xhaka anaamini kwamba, Mikel Arteta ndiye mtu sahihi wa kuipeleka mbele klabu hiyo.

Matumaini ya Washika Bunduki hao kutwaa taji la Ligi Kuu ya England yalimalizika Jumamosi (Mei 20) walipopoteza 1-0 dhidi ya Nottingham Forest, ambao walishuhudia Manchester City wakitawazwa mabingwa kwa mara ya tano ndani ya misimu sita.

Lakini walikaa kileleni mwa ligi kwa siku 248 za msimu na walikuwa na uongozi wa alama nane dhidi ya City Machi, lakini licha ya kuchelewa kwao kushika nafasi ya kwanza kikosi cha Arteta kimepata sifa kwa maendeleo yao msimu huu.

Alipoulizwa kama alidhani Arteta ndiye angeweza kuwaongoza katika harakati za kuwakimbiza City, alisema: “Unaweza kusahau swali hilo yeye ni zaidi ya kocha sahihi wa timu hii.”

Arsenal wamepoteza vibaya katika mechi zao nane zilizopita, wakishinda mara mbili pekee, lakini Xhaka amesema msimu huu un- apaswa kuwa msingi wa kusonga mbele.

“Hatuhitaji kusahau jinsi tulivyofanya kazi kwa miezi 11 iliyopita,” alisema.

“Hata tulipopoteza katika michezo miwili iliyopita, bila shaka watu wanaona kinachotokea sasa, lakini usisahau miezi 11 tuliyofanya kazi.

“Ikiwa mtu alituambia kabla ya msimu kuwa tutakuwa hapa, nadhani kila mtu asingeamini. Lengo letu la uhakika lilikuwa kurejea katika nafasi nne za juu. Sasa sisi ni wa pili. Bila shaka unapokuwa karibu sana na taji unataka kushinda taji.

“Lakini tupo pale tulipo, tunastahili kuwa hapa tulipo, na tuone nini kitatokea msimu ujao. Tunapaswa kwenda na kufanya hatua inayofuata.”

Chanzo: Dar24