Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gor Mahia Mabingwa Ligi Kuu Kenya 2023/24

Gor Mahia Winning Gor Mahia Mabingwa Ligi Kuu Kenya 2023/24

Mon, 20 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Gor Mahia imeshinda taji la 21 la Ligi Kuu ya soka ya Kenya baada ya ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Muhoroni Youth, na kutinga kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika 2024/2025.

Ushindi huo uliinua timu hiyo maarufu kama ‘K’Ogalo’ baada ya kujikusanyia uongozi usioweza kuepukika wa pointi 67, pointi 11 mbele ya Tusker iliyo nafasi ya pili zikiwa zimesalia mechi tatu ili Ligi kuu imalizike.

Mshindi wa kiatu cha dhahabu Benson Omalla alifunga bao lake la 16 msimu huu katika kipindi cha mapumziko Gor Mahia wakiwa mbele kwa bao 1-0 hadi mapumziko.

Kushinda Ligi hiyo pia kumeifanya Gor kukata tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya CAF msimu ujao.

Kwa upande mwingine, mbio za Muhoroni Youth kuepuka kushuka daraja zilipata pigo kubwa baada ya kushindwa na Mabingwa hao.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live