Wed, 20 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Golikipa wa Lazio Ivan Provedel jana kwenye usiku wa UEFA alifunga goli dakika za mwisho kabisa na kuinusuru timu yake kipigo wakiwa nyumbani kutoka kwa Atletico Madrid hivyo mchezo kutamatika kwa sare ya 1-1.
Sio mara ya kwanza kwa mlinda lango huyo kufunga dakika za lala salama na kunusuru timu yake na kichapo, mwaka 2020 aliifungia kwa kichwa timu yake ya Juve Stabia goli la pili katika sare ya 2-2 dhidi ya Ascoli kwenye Serie B.
Huyu unaweza kumfananisha na kipa gani hapa bongo?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live