Golikipa wa ‘klabu’ ya Barcelona, Marc Andre Stegen anadaiwa kutoonekana kikosini kwa takribani miezi miwili, kwani anatarajia kufanyiwa upasuaji wa jeraha dogo la mgongo hivi karibuni.
Golikipa wa ‘klabu’ ya Barcelona, Marc Andre Stegen anadaiwa kutoonekana kikosini kwa takribani miezi miwili, kwani anatarajia kufanyiwa upasuaji wa jeraha dogo la mgongo hivi karibuni. Nafasi yake itachukuliwa na mlinda mlango Inak kwa kipindi chote ambacho Marc atakuwa nje ya kikosi na inadaiwa kuwa ‘klabu’ hiyo haina mpango wa kusajili goli kipa mwingine sababu wanaamini mlinda mlango aliyebakia atatosha kuisaidia ‘timu’.