Rais wa shirikisho la soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe amekiri kuwa goli la Yanga lililokataliwa mwamuzi katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Mamelod Sundowns Afrika Kusini lilikuwa goli halali.
Rais Motsepe ameyasema hayo leo alipowasili visiwani Zanzibar katika fainali za African schools football na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa TFF Wallace Karia.
“Japo Rais wa CAF hatakiwi kutoa maoni yoyote kuhusu maamuzi ya mwamuzi lakini kwangu mimi nilivyorudia kuangalia lilikuwa ni goli halali” — amesema Motsepe.
Motsepe: Goli la Aziz Ki lilikuwa halali
— TBCOnline (@TBConlineTZ) May 24, 2024
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Patrice Motsepe amesema goli walilofunga Yanga SC dhidi ya Mamelodi Sundowns lililokataliwa lilikuwa halali. pic.twitter.com/YZtyMr7Zhs