Fri, 4 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mlinzi wa Barcelona, Gerard Pique ametangaza kuwa atastaafu soka akiwa na umri wa miaka 35 huku mechi ya Jumamosi ya Barcelona dhidi ya Almeria ikiwa ndio ya mwisho kwake Camp Nou.
Pique ambaye amekuwa na wakati mgumu kupata nafasi ya kucheza chini ya Xavi msimu huu leo Alhamisi ameamua kuwa sasa inatosha.
Beki huyo amejitengenezea heshima kubwa kama mmoja wa mabeki bora wa kizazi chake baada ya kurejea Barcelona kutoka Manchester United mnamo 2008.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live