Sat, 2 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mpenzi wa mchezaji Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez ameonesha kumsapoti, na kumpa heshima mpenzi wake huyo kwa kuvalia vazi lililoandikwa jina la #CR7 katika maonesho ya mavazi ya ‘Vetements Fall/Winter’ yaliyofanyika usiku wa kuamkia leo jijini Paris.
Georgina alivaa gauni jekundu yenye jina la mpenzi wake pamoja na namba saba ambayo Cr7 amekuwa akiivaa toka yupo Real Madrid.
Cristiano Ronaldo na Georgina Rodriguez wapo katika uchumba kwa muda mrefu, wanaishi na watoto watano ambao baadhi yao ni watoto wa nje wa #Cr7.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live