Mechi kati ya wenyeji Geita Gold Fc dhidi ya Yanga Sc itapigwa katika uwanja wa CCM KIRUMBA, Mwanza Jumapili hii Machi 6
"Ule mradi wetu wa uwanja bado haujakamilika, tunatarajia kufikia mwezi wa nne utakuwa umekamilika, uwanja tunaotumia kwa sasa ni mdogo auwezi kukidhi washabiki wote wa kanda ya ziwa kwaio tumeona tuje Mwanza uwanja wa CCM Kirumba, ukizingatia geita Gold ipo kanda ya ziwa na imetokana na Mwanza"
"Niwaombe tuu mashabiki wote wa Kanda ya ziwa na wa mikoa ya jirani wajitokeze kwa wingi kuja kuishuhudia burudani hii"
katibu Mkuu wa timu ya Geita Gold'Simon Shija' akielezea sababu za kuuleta mchezo wao dhidi ya Yanga uwanja wa CCM Kirumba na sio Nyankumbu tena.