Mon, 20 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la soka Duniani FIFA limeitaka klabu ya Geita Gold kumlipa kiasi cha Million 10 mchezaji wake wa zamani wa klabu hiyo Shawn Oduro, kiasi ambacho anaidai klabu hiyo.
Geita Gold imepewa siku 45 ili iwe imekamilisha zoezi la malipo kwa beki huyo lasivyo itakutana na rungu la kufungiwa kufanya usajili.
Beki huyo kisiki raia wa Ghana alisajiliwa na Geita Gold kwenye dirisha kubwa la usajili msimu uliopita wa 2022/23.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live