Leo ni moja ya siku ambayo mashabiki na wapenda soka wanatamani muda ukimbie kwa hamu ya kutamani kuona mtanange baina ya Kaizer Chiefs dhidi ya Yanga.
Miamba hiyo itashuka dimbani saa 10:00 jioni katika mechi ya Toyota Cup itakayopigwa nchini Afrika Kusini.
Kaizer kwa sasa inanolewa na aliyekuwa wa Yanga, Nasreddine Nabi ambaye aliacha alama kubwa Jangwani baada ya kuwafikisha fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga kwa sasa inanolewa na Kocha Miguel Gamondi ambaye amejitengenezea umwamba wake baada ya kuwafikisha robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika na kuchukua mataji mawili ya LigI Kuu Bara.