Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gamondi kazi anayo Yanga

Pacome, Nzengeli, Nkane Wachezaji wa Yanga

Sun, 27 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hakuna kitu kizuri kama kuiangalia Yanga ya Gamondi ikicheza, kama unadaiwa kodi, una njaa, una uchovu ama unaumwa homa ndogondogo basi ni dawa inayotibu kwa dakika 90 tulizoshuhudia pale Azam Complex, Chamanzi.

Hakuna kitu kigumu hivi sasa kama kutabiri kikosi cha Yanga kitakachoanza, kila mchezaji anapata nafasi na anakupa kile unachohitaji kwa ubora wa hali ya juu.

Hakuna kitu kigumu kama kutaja man of the match kwenye mchezo wa leo kutokana na namna wachezaji wote walivyomwaga jasho kuipigania bendera ya kijani na njano.

Sio Kibwana aliyekosa michezo kadhaa, sio Mkude aliyekua Morogoro kwenye mechi mbili za nyuma, sio Sure boy aliyekaa benchi mechi mbili, sio Max , sio Kibabage, sio Pacoume aliyeingia kutokea Sub, sio Azizi ki aliyezaliwa upya msimu huu, wala sio Mzize ambaye hakuwepo hata sub kwenye mchezo uliopita kila mmoja anakiwasha.

Hapo bado man of the match kwenye mchezo dhidi ya KMC, Mudathir yuko benchi mtawala wa dimba la kati Doctor Khalid Aucho yuko jukwaani, Yao Attouhoula, Lomalisa, Kenedy Musonda.

Beki bora wa Ligi msimu uliopita na captain kwenye mchezo dhidi ya KMC Dickson Job wanaitazama mechi kwenye TV na bado Asas kala Mkono na mpira mwingi.

Hakuna mtihani mgumu kama kuwa Gamondi, uanze na mchezaji yupi na yupi akae benchi, kila anayepata nafasi anacheza.

Hakuna kitu kigumu kama kukabiliana na ile pressing ya Yanga kuanzia highline, kutoka dakika ya kwanza mpaka 90, wanakuja tu kama wana ugomvi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: