Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe amemkabishi Diary Afisa Habari wa Singida Fountain Gate Hussein Massanza ambayo ina mifumo (mbinu za mchezo) mitatu ambayo itawasaidia Singida kuifunga Future FC kwenye mchezo wao wa Shirikisho Barani Afrika.
Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe amemkabishi Diary Afisa Habari wa Singida Fountain Gate Hussein Massanza ambayo ina mifumo (mbinu za mchezo) mitatu ambayo itawasaidia Singida kuifunga Future FC kwenye mchezo wao wa Shirikisho Barani Afrika. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Septemba 12, 2023, Kamwe amesema kuwa wao kama Yanga wametoa hiyo kama sapoti kwa Singida ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha nchi inafanikiwa katika michezo yote ya kitaifa.