Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gamondi awaonya mastaa wake

Gamondi Chama Aziz Pacome Gamondi awaonya mastaa wake

Tue, 10 Sep 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Licha ya kikosi chake kuonyesha ubora mkubwa katika mechi za mwanzo msimu huu, Kocha Mkuu wa Yanga Sc Miguel Gamondi amesema haimaanishi kama wako salama na itakuwa rahisi kwao kupata mafanikio kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Gamondi amesema msimu huu anatarajia kupata upinzani mkali zaidi kutoka kwa wapinzani wao katika michuano yote wanayoshiriki kwani kila timu inajiandaa kwa lengo la kushindana na Yanga Sc.

"Kila timu sasa inataka kuifunga Yanga Sc, inabidi tupambane, tusijidangaye kuwa tupo kwenye mstari salama, ninawaambia haya hata wachezaji wangu, wanatakiwa kila siku waongeze juhudi na mazoezi zaidi ili tuwe bora kila kukicha kwani wenzetu nao wanaongeza ubora ili watufikie au watupite."

Nini Maoni Yako Mdau wa Soka?

Chanzo: www.tanzaniaweb.live