Wakati Medeama wakijipanga kunavaana na Yanga kesho kuanzia saa 1:00 usiku, kocha wa Yanga, Miguel Gamondi amepenyezewa taarifa nzito ambayo haraka ameanza kujipanga nayo.
Gamondi alisema anafahamu Medeama kikosi chao kitakuwa na mabadiliko makubwa kwenye eneo lao la ushambuliaji kufuatia kurejea kwa mshambuliaji wao mahiri Jonathan Sowah.
Gamondi amelifichulia Mwanaspoti, Sowah ndio mshambuliaji hatari kwenye kikosi cha Medeama ambapo kesho atarejea uwanjani baada ya kukosa mechi iliyopita kwa kuwa na kadi tatu za njano na tayari ameshawapanga vijana wake kukabiliana naye na wengineo wote jijini Kumasi.
“Anaweza kufunga kwa njia mbalimbali kuanzia mabao ya kichwa na hata miguu.”