Baada ya kutoka suluhu ya 0-0 kati ya CR Belouizdad na Al Ahly sasa ni rasmi kuwa Yanga itakuwa na wakati mgumu wa kufuzu hatua ya robo fainali ukilinganisha na wapinzani waliobaki kwenye kundi lake.
Al Ahly ni kinara wa kundi hilo
Al Ahly - pts6
CR Belouizdad -pts 5
Yanga SC - pts5
Medeama SC -pts4
Yanga na CR Belouizdad zinalingana alama lakini utofauti wao ni magoli ya kufunga na kufungwa na kulingana na mechi zilizosalia Yanga ina wakati mgumu zaidi wa kufuzu hatua inayofuata.
Mchezo utakaoamua hatma ya Yanga ni ule dhidi ya CR Belouizdad utakaopigwa kwenye dimba la Mkapa, Jijini Dar Es Salaam, Gamond ana wakati mgumu sana hapa.
MECHI ZIJAZO
Medeama SC vs Al Ahly
Yanga SC vs CR Belouizdad