Wakati Yanga ikijindaa kuwavaa Azam FC leo Uwanaja wa Mkwakwani Jijini Tanga katika michezo ya mtoano kuwania Ngao ya Jamii.
Kocha Mkuu Yanga, Miguel Gamondi ameonekana kuingiwa na wasiwasi akitazama namna mpinzani wake alivyo imara.
Akizungumza Gamondi amesema; . “Sijaiangalia sana Azam ikicheza, nafahamu walikuwa nje ya nchi, tutaingia uwanjani kwa tahadhari kubwa, wachezaji wangu wanafahamu nini cha kufanya na wameonekana kuelewa vizuri mbinu zangu,” . “Kitu kizuri wachezaji wangu wote wapo kwenye ari nzuri, nina uwiano mzuri wa wachezaji wale watakaoanza na watakaokaa kwenye benchi, hili litanipa eneo kubwa la kuchagua nani aanze na mbinu gani nitumie kupata matokeo mazuri,” alisema Gamondi.