Wakati Mashabiki wakilalamikia kiwango cha Straika wa Yanga Joseph Guede kwa kuona hana mchango katika kikosi chao.
Kocha Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi amesema mchezaji huyo ni muhimu katika kikosi chake kuelekea michezo iliyopo mbele yao.
Akizungumza Gamondi anasema;
“Siwezi kuacha kumtumia Guede (Joseph) bila sababu ni mchezaji mzuri na ana mchango mkubwa kwa timu, umakini wake unaanzia mazoezini, naamini ataendelea kupata nafasi atafanya makubwa sana msimu huu, binafsi namuona ni straika hatari,”
“Tunaenda kwa kumheshimu mpinzani (Mamelodi Sundowns) tunatarajia ushindani lakini tumejiandaa kusaka ushindi muhimu kurudisha morali ya wachezaji baada ya kupoteza mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Azam FC,”