Novemba 5 saa 11 jioni, Simba na Yanga zitakwaana kwa mara ya kwanza kwenye mechi ya Ligi msimu huu ndani ya Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.
Mpaka sasa wanalingana pointi kwenye msimamo huku zikitofautiana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa, lakini makocha wa timu hizo, Miguel Gamondi na Roberto Oliveira ‘Robertihno’ wamechimba mkwara mzito kusisitiza ni mechi kubwa na ngumu lakini pointi tatu zipo.
Kocha wa Yanga, Gamondi ambaye ni Muargentina amesema wanakwenda kumalizia maandalizi yao ya mchezo mkubwa ambao uko mbele yao akijua wapin-zani wao walimpokonya taji la Ngao ya Jamii.