Wed, 4 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Yanga SC, Gael Gamondi amesema hawalaumu waamuzi wa mchezo wao wa leo dhidi ya Ihefu FC bali anawalaumu wachezaji wake kwa kushindwa kufunga.
Amesema, amechukizwa na matokeo hayo lakini ndio mpira hivyo wanajiandaa na mchezo ujao.
"Hatulaumu marefa kwa ksuhindwa kuamua japo tumeona lulikuwa na matatizo mengi kama wachezaji kupoteza muda, kujiangusha lakini tunajilaumu sisi kwa kushindwa kuweka mpira wavuni," alisema Gamondi.
Mchezo huo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa katika uwanja wa Highland Estate ulimazika kwa Yanga kufungwa 2-1.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live