Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gadeil Michael anasaka timu Sauzi

Gadiel Michael Kamagi.jpeg Gadeil Michael anasaka timu Sauzi

Thu, 15 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Beki wa kushoto wa kiwango cha juu wa Fountain Gate Gadiel Kamagi bado yupo katika soko la uhamisho, imethibitishwa.

Beki huyo wa kushoto alicheza nafasi kubwa katika kikosi cha Ernst Middendorp katika klabu ya Cape Town Spurs msimu uliopita ambapo alifunga mabao 4 na kutoa pasi 4 za mabao kwenye mashindano ya DSTV Premiership.

Beki huyo wa Tanzania alikaribia kusaini Kaizer Chiefs hadi dili la Bongani Sam lipolikamilishwa rasmi na wababe hao wa Afrika Kusini.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 anaripotiwa kutokuwa na nia ya kurejea katika klabu yake ya Fountain Gate, na pia amekataa ofa ya kurejea Cape Town Spurs iliyoshuka daraja ambako alikuwa akiichezea klabu hiyo kwa mkopo.

AmaZulu, Chippa United na Sekhukhune FC walikuwa wakimtaka. Gadiel amewahi kuichezea Azam FC, Yanga kabla ya kutimkia Simba SC na baadaye Singida Fountain Gate FC.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: