Fri, 27 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal Gabriel Jesus atafanyiwa vipimo leo huku Arsenal ikitafuta kujua ukubwa wa jeraha lake la msuli wa paja,
Mbrazil huyo alisema baada ya mchezo huo kumalizika kuwa ana uhakika jeraha hilo si kubwa lakini hana uhakika kama atakuwepo kwenye mchezo wa Jumamosi wakiwa nyumbani dhidi ya Sheffield United inayoshika mkia kwenye Ligi Kuu ya Uingereza.
Arsenal walikaa hispania usiku wa kuamkia Jumanne na kumfanyia matibabu na Jumatano asubuhi walirudi Uingereza, huku kikosi kikishiriki mazoezi ya Alhamisi kama kawaida.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live