Staa wa ngumi uzito wa juu duniani, Tyson Fury, amewaunga mkono mabondia wa Ukraine, Wladimir Klitschko na Vitali Klitschko kwa kitendo cha kujitoa kwenda kusapoti nchi yao katika vita inayoendelea.
Mabondia hao ambao ni ndugu wamejitoa kwenda kupambania nchi yao ya Ukraine ambayo ipo kwenye vita dhidi ya Urusi.
Mwaka 2015, Fury alifanikiwa kupambana na bondia mmoja kati yao ambaye ni Wladimir Klitschko, akashinda.
Staa huyo alisema: “Kuna sheria mbili, mpende mwanamke wako na pambania nchi yako, hivyo wacha wapambanie nchi yao jambo ambalo ni muhimu, mimi niko pamoja nao.
“Kwa sababu unaweza kutafuta fedha halafu mwisho wa siku ukashindwa kurudi nyumbani na kutamba, hivyo ni bora kwenda kuipigania nchi yako. “Vijana endeleeni kupambana bila kuchoka na wala msikate tamaa, msijisalimishe, tuko pamoja.”