Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Fundi mwingine Liverpool atajwa Saudi Arabia

Ibra Konate Fundi mwingine Liverpool atajwa Saudi Arabia

Wed, 30 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ibrahima Konate amekuwa mchezaji wa hivi punde zaidi wa Liverpool kupewa nafasi ya kuhamia Saudi Arabia, kwa mujibu wa RMC Sport.

Liverpool iliwapoteza Jordan Henderson na Fabinho kwenye Ligi Kuu ya Saudia na wanapigania kumbakisha Mohamed Salah huku kukiwa na tetesi za ofa kubwa kutoka kwa Al-Ittihad.

Alisson na Joe Gomez pia wamehusishwa na kuhamia Mashariki ya Kati. Sasa Al-Ittihad inaripotiwa kumsikiza Konate baada ya kukataliwa na Jean-Clair Todibo wa Nice. Konate ana furaha akiwa na Liverpool, ambao hawataidhinisha uhamisho huu mwishoni mwa dirisha la usajili.

Hivi majuzi iliripotiwa kuwa Konate pia alikataa nafasi ya kuhamia Saudi Arabia, huku Hawkins akieleza kuwa “anajisikia vizuri akiwa Liverpool ambapo anataka kufikia malengo yake.”

Wakati deadline imeongezwa hadi Septemba 7 nchini Saudi Arabia, dirisha litafungwa kwa vilabu vya Premier League saa 11 jioni siku ya Ijumaa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: