Fri, 3 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Juventus Paul Pogba, amerejea uwanjani baada ya kukosekana kwa miezi kadhaa kutokana na majeraha yaliyokuwa yanamkabili.
Pogba alijiunga na Juventus mwanzoni mwa msimu huu akitokea Manchester United ambako alidumu kwa miaka mitano.
Licha ya usajili wake hajapata nafasi ya kucheza kutokana na kusumbuliwa na majeraha yaliyomfanya kukosa mpaka Michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyoika Qatar.
Aliingia kutokea Benchi kwenye mchezo walioshinda bao 4-2 dhidi ya Torino.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live