Tue, 5 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa zamani wa Chelsea na timu ya Taifa ya Ufaransa Frank Leboeuf anaamini kuwa Ureno haitaweza kuchukua Euro 2024 ikiwa na Cristiano Ronaldo.
Leboeuf anasema kama Ureno haitamjumuisha Ronaldo kwenye kikosi chao basi dhahiri wanaweza kuwa washindani wa kombe la Ulaya [Euro 2024].
"Kwangu mimi, Ureno ni miongoni mwa timu zitakazokuwa kwenye nafasi ya ubingwa wa Euro 2024 majira haya ya joto."
"Nafikiri wanaweza kuwa mabingwa wa Euro, lakini kama tu Cristiano Ronaldo hatacheza."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live