Nyota wa klabu ya Manchester City Phil Foden ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa EPL iliyotolewa na waandishi wa habari [FWA'S Footballer of the year Awards].
Kwa upande wa wanawake nyota wa klabu ya Manchester City Khdaija 'Bunny' Shaw ameshinda tuzo hiyo akimshinda Laurien James dada yake Reece James.
Hii inakuwa mara ya kwanza kwa wachezaji wawili wa Manchester City kutwaa tuzo hiyo tangu walivyofanya hivyo Nikita Parris na Raheem Sterling mwaka 2019.
Foden ni nyota wa tatu wa Manchester City kutwaa tuzo hiyo kwa miaka minne mfululizo.Mwaka 2021 alitwaa Ruben Dias na 2023 akitwaa Erling Haaland