Sat, 18 May 2024
Chanzo: Mwanaspoti
Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Manchster City, Phil Foden ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa msimu wa Ligi Kuu ya England kwa msimu wa 2023/2024 baada ya kufunga magoli 17 na kusaidia (assist) mengine 8 kwenye Ligi hiyo msimu huu.
Foden anakuwa mchezaji wa tano wa Man City kutwaa tuzo hiyo kwa msimu wa tano mfululizo kuanzia msimu wa 2019/20.
Washindi wa Tuzo ya mchezaji bora wa msimu kwa misimu mitano iliyopita
2019/20, Kevin De Bruyne
2020/21, Ruben Dias
2021/22, Kevin De Bruyne
2022/23, Erling Haaland
2023/24, Phil Foden
Chanzo: Mwanaspoti