Nguli wa Ureno Luis Figo amekosoa uamuzi wa kocha wa timu ya Taifa Ureno wa kumuacha Cristiano Ronaldo nje ya kikosi kilichoanza kwa mara ya pili juzi katika mchezo wa robo ya kombe la Dunia 2022 dhidi ya Morocco.
Nguli wa Ureno Luis Figo amekosoa uamuzi wa kocha wa timu ya Taifa Ureno wa kumuacha Cristiano Ronaldo nje ya kikosi kilichoanza kwa mara ya pili juzi katika mchezo wa robo ya kombe la Dunia 2022 dhidi ya Morocco. “Huwezi kushinda kombe la Dunia Ronaldo akiwa benchi. Sawa timu ilishinda dhidi ya Uswisi! Matokeo mazuri lakini unaweza kufanya hivyo kila mechi? Hapana. Kumuacha Ronaldo nje lilikuwa kosa, kufungwa huku kwa timu ( kipigo dhidi ya Morocco) kumesababishwa na uongozi wa timu na kocha ” amesema Figo.